Kilimo bora cha Dengu


UTANGULIZI
Dengu ni zao la chakula na biashara lenye kiasi kikubwa cha protini, vitamini A na B, Madini ya Potassium na chuma. 
Zao hili likilimwa vizuri linaweza kutoa mavuno ya kilogram 200 hadi 500 kwa ekari.Zao hili huchukua wastani wa siku 135 kupandwa hadi kuvunwa.

HALI YA HEWA NA UDONGO
Ni zao linalohitaji hali ya hewa ya kibaridi kiasi kwani joto kali na ukame sana huathiri mavuno yake,hupunguza wingi wa mavuno. 
Ni zao linalostahimili ukame,linaweza kukua katika hali ya hewa ya unyevunyevu tu.Kama utakuwa unamwagilia basi epusha unyevu mwingi ikifikia kipindi cha maua hadi kuvuna.Zao hili linaweza kulimwa katika udongo wa aina tofauti tofauti wenye P.H 6-8.Udongo wenye asidi na base kidogo.Kwa Tanzania zao hili linaweza kulimwa katika mikoa ya Iringa,Dodoma,Mwanza,Singida,Morogoro N.K 

UPANDAJI NA NAFASI
Zao hili huitaji mbegu kiasi cha kilogram 15 hadi 40 kutegemea ukubwa wa mbegu husika. 
Zao hili hupandwa mwishoni mwa msimu wa mvua,unaweza kupanda baada ya kuvuna mazao mengine uliyopanda mapema, 
Mbegu za dengu hufukiwa katika kina cha sentimeta 4 hadi 6 ili kufanya mazingira rafiki kwa bacteria wa rhizobia kufanya kazi.Zao hili usipande pamoja na vitunguu na tangawizi.Panda kwa kutumia drilling method-njia ya vifereji kwa nafasi ya mistari miwili ya sentimeta 15 na sentimeta 30 hadi 50 kwa mstari hadi mstari.

MBOLEA ZA VIWANDANI NA SAMADI
Mbegu unaweza kuzipanda baada ya kuziongeza inoculam kundi F na Pia Mbolea ya DAP kilogram 25 hadi 50 kwa ekari katika shamba lisilo na rutuba ya kutosha.

PALIZI-Palilia mapema shamba lako.

WADUDU WAHARIBIFU KWA DENGU
Dengu hushambuliwa na Mchwa wakubwa weusi,aphid wa njegere,funza wa vitumba,Inzi wa lucina n.k
wazuie wadudu hawa kwa kupuliza dawa za wadudu mara tu uonapo dalili za mashambulizi ya wadudu.

MAGONJWA YA DENGU
Dengu hushambuliwa sana na magonjwa ya ukungu ambayo.Hivyo kama eneo lako hushambuliwa na ukungu mara kwa mara basi puliza dawa za ukungu (FUNGICIDES)


UVUNAJI WA DENGU
Zinavunwa mara tuu pindi vitumba vya chini vibadilikapo rangi kuwa kahawia angavu na vitumba vikiguswa hutoa sauti.

No comments:

Post a Comment

UJENZI WA BANDA LA KUKU

Ujenzi wa mabanda bora ya kuku ni miongoni mwa mambo ya msingi kabisa katika ufugaji bora wa kuku wawe ni wa asili au wale walioboreshw...