Kilimo Cha Mbaazi Tanzania


Mbaazi ni moja kati ya mazao yanayo limwa kwa wingi nchini Tanzania 
Hali ya hewa  inafaa kwa kilimo kwa kilimo mbaazi ni nyuzi joto 18 hadi 38sentigredi.mbaazi huwa hazivumialii barafu .Mbaazi hustawi kwenye mvua kwa mwaka kiasi cha milimita 600 hadi 1000 inagawa aina za muda mfupi hustawi kwenye kiwango kidogo cha mvua milimita 250.hazistawi zaidi kwenye usawa wa bahari
AINA ZA MBAAZI
Kuna makundi makuu matatu ya zao la mbaazi

MBAAZI ZA MUDA MREFU


Huchukua miezi sita mpaka saba shambani mpaka wakati wa kuvuna.
Zina matawi machache na ni ndefu hvyo hufaa sana kwa kilimo mseto.haini zinaweza kuvunwa zaidi ya msimu mmoja lakini mazao yanayopatikana baada ya msimu wa kwanza huwa madogo hivyo inashauriwa aina zipandwe upya kila mwaka
USTWAI;Aina hizi hustawi vizuri katika ukanda wa juu na kati wenye mvua za kutosha .

MBAAZI ZA MUDA WA KATI

SIFA ZAKE
Hukomaa ndani ya muda wa miezi minne na nusu mpaka miezi sita baada ya kupandwa.zina matawi mengi na ni fup kulingana na mbaazi za muda mrefu.hazikomai zote kwa wakati mmoja humlazimu mzalishaji kuvuna zaidi ya mara moja ingawa mazao ya kwanza ni mengi kuliko mazao yanayofata.zinapendwa na kina mama kwa sababu ya mboga kwa jili ya mboga au enderefu kwa sababu huchanua tena mara zikipata maji
USTAWI;Aina hii ya mbaazi hulimwa katika ukanda wa kati mita 800 hadi 1100 usawa wa bahari zenye mvua za wastani

MBAAZI ZA MUDA MFUPI
Kundi hili linawakilisha aina bora za mbaazi za muda mfupi yaani miezi 3 hadi 3 na nusu.


SIFA ZAKE

Aina hii ni fupi ni mita moja hadi moja na nusu yenye mauwa mekundu inapoanza kuchanua hulimwa katika ukanda wa kati na wa chini katika uhaba wa mvua kama vile maeneo ya pwani
Aina hii hazichanganywi na mahindi ,inahatari ya kushambuliwa sana na wadudu hasa ukanda wa kati na wa juu sababu huchanua wakati wa mvua
Tofauti na aina zote za mbaazi aina hii haiasiliwi nan a urefu au ufupi wa siku hivyo itachanua wakati wowote mara baada tu ya kupanda
Haina hii ya mbaazi haina ukinzani wa ugonjwa wa kunyauka

MATUMIZI YA MBAAZI
Chakula kwa binadamu
Kilimo cha mseto,mbaazi za muda wa kati na muda mrefu zinaweza kulimwa mseto na mzao mengine ya jamii ya nafaka mfano mahindi , mtama ,uwere
FAIDA ZA KULIMA MBAAZI NA MAZAO MENGINE
1 Matumizi bora ya ardhi hasa kwa kuwa mbaazi huongeza ufyonzaji wa hewa ya naitrogen shambani
2 Mzalishaji atapata mazao mawili au zaidi katika shamba mojana msimu mmoja
3 Kipato cha mzalishaji kitaongezeka kutokana na mazao mengine
4 Pia mafuno ya mazao ya nafaka kama mahindi hayapungui kwa kiasi kikubwa kutokana na mchango huo wa mazao

UTAYARISHAJI WA SHAMBA
1 N’goa visiki pamoja na mabaki yote ya mimea kabla ya uzalishaji
2 Lainisha udongo kwa kupiga halo mbaazi zinavyoota huwa dhaifu sana na kama shamba halikuandaliwa vizuri magugu huota mapema kabla ya mbegu za mbaazi
3 Tayarisha matuta au makinga maji kama shamba lipo kwenye mteremko .



KUANDAA MBEGU
Mbegu bora iliyochaguliwa vizuri na kuhakikiwa kiwango cha uwotaji iandaliwe
 Mbegu ziwekwe dawa za kuzuia kuvu kabla ya kupanda ili kuzuia magonjwa yatokanayo na mbegu na udongo
MBEGU BORA
Mbegu za mbaazi zimegawanywa kwenye makundi makuu matatu
1 mbegu ya mda mfupi
2 mbegu ya mda wa kati
3 mbegu ya mda mrefu
UOTESHAJI
Nafasi kutoka mstari hadi mstari hutegemea zao kuu linalopandwa .kilimo mseto na mahindi hutegemeana pia na aina za mbegu sentimita 90 mpaka 120 sentimita unashauliwa kutoka mstari hadi msatri 50 sm kutoka shimo hadi shimo acha mimea miwili kwa shimo
Panda mahindi yanayo komaa mapema ili yavunwe mapema na kutoa nafasi kwa mbaazi ili kuchanua na kutanuka
Tumia kilo 4 hadi 5 kwa hekari kutegemeana na ukubwa wa punje
 UPANDAJI
Mbaazi za mda mrefu panda kwa mistari kwa umbali wa sm150 kwa sm100
Mbaazi za muda wa kati panda kwa mstari wa sm100 kwa 60sentimita
Mbaazi panda kwa umbali wa nafasi sm90kwa 60sentimita
MBOLEA
Mbaazi hustawi vizuri kwenye shamba lenye mbolea ya kutosha.Hivyo inapendekezwa kwamba kila mzalishaji aweke mbolea ya samadi ili kuhifadhi arhdi dhidi ya upotevu mkubwa wa mbolea
Jamii ya mikunde hujitengenezea aina ya mbolea ya naitrogen . hata hivyo tafiti zinaonesha kwamba matumizi ya mbolea za kupandia kama mabolea ya minjigu ,TSP,OAP,kutaimarisha mizizi na mshina na hivi kuongeza uzalishaji

PALIZI NA KUPUNGUZA MIMEA
Ni muhimu kuoalilia mapema kuondoa magugu ambayo hushindana na mimea .palizi ifanyike mara mbili kwa wakati.palizi tatu inategemea wingi wa majani na unyevu au mvua . mishe ikiwa mingi kwenye shina husabsbisha mazao kidogo kutokana na mimea kushindania mwanga na virutubisho. Palizi inaweza kufanyika kwa jembe la mkono au trector kulingana na nafasi iliyotumika katika kupanda . palizi mbili za mwanzo kati ya siku 60 za mwanzo ni muhimu kbla ya mbaazi hazijawa na kivuli cha magugu kumea lakini pia kiuwa gugu kinaweza kutumika kabla ya mbaazi kuota .baada ya mbaazi kuota dhidi ya magugu ya majani mapana ichanganywe Fluazifopbutyl kudhibiti magugu jamii ya nyasi,kiuwa gugu kitumike wakati mbaazi zimekua kufikia sentimita 25 hadi 30 .Nimuhimu kupunguzia miche na kubakiza miwili au kutegemeana na nafasi iliyo tumika
  
UVUNAJI WA MBAAZI
Mbaazi zikisha komaa na kuanza kukauka zivunwe mapema kwa kukatwa matawi yenye mbaazi na kukausha zaidi kisha mbaazi zitenganishe kwa mikono au kwa kupigwa hayo mati taratibu baada ya kukaushwa sana

No comments:

Post a Comment

UJENZI WA BANDA LA KUKU

Ujenzi wa mabanda bora ya kuku ni miongoni mwa mambo ya msingi kabisa katika ufugaji bora wa kuku wawe ni wa asili au wale walioboreshw...